Thursday, May 16, 2013

Huduma za Upimaji Ramani



Majukumu ya Idara kwa Ujumla

Majukumu ya Idara

Upimaji na Ramani ni Idara katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi. Jukumu lake kubwa ni usimamizi wa upimaji ardhi na utayarishaji wa ramani na plani mbalimbali za nchi mijini na vijijini. Ramani hizo ni msingi wa kubuni, kutekeleza na kuratibu mipango ya maendeleo juu ya ardhi katika sekta na kwa matumizi mbalimbali kama:

  • Umilikishaji ardhi
  • Kupanga matumizi ya ardhi
  • Utalii
  • Mawasiliano
  • Makazi
  • Kilimo
  • Hifadhi ya mazingira
  • Utafiti na uchimbaji madini

2.   Bidhaa zinazouzwa

Description: http://www.ardhi.go.tz/sites/default/files/clip_image002.jpg
Urasimu ramani

2.1   Ramani.

Ramani   za   msingi   kutokana   na picha za anga (base maps):

  • Ramani za topografia za skeli ya kati 1:50,000 kwa nchi nzima  
  • Ramani za maeneo ya mijini katika skeli ya 1:2,500 au 1:5,000

Ramani za kuzalisha kutokana na ramani za msingi  

  • Ramani katika skeli ya1:250,000 
  • Ramani za Mikoa na Wilaya katika skeli kati ya 1:300,000 -1:500,000
  •           Ramani za masomo maalum
  • Ramani ya Barabara ya Tanzania katika skeli 1:2m 
  • Ramani yaTawala za Mikoa na Wilaya katika skeli ya l:2m 
  • Ramani ya Jiji la Dar es Salaam katika skeli ya I :20,000 
  • Ramani ya Utalii ya Mlima Kilimanjarokatikaskeli ya 1:1 00,000

2.2 Picha za Anga

Idara ya upimaji na ramani ina maktaba ya picha za anga za sehemu mbalimbali za nchi zilizopigwa katika       nyakati mbalimbali tangu miaka ya 1940. 

  • Picha za ,skeli ndogo chini ya 1:50,000

  • Picha za skeli ya kati I :20,000   1:50,000
  • Picha za skeli kubwa zaidi ya 1:20,000

2.3 Takwimu na kumbukumbu za

Upimaji Ardhi.

Idara ni mhazini wa takwimu na kumbukumbu   za   upimaji   miliki nchini

  • Kadi za vielelezo vya alama za msingi za upimaji 
  • Vipimo vya alama za msingi za upimaji
  • Plani za upimaji miliki

2.4 Bidhaa Maalum

Idara    ina    uwezo    kivifaa    na kitaaluma   kutayarisha   ramani, na kutoa huduma mbalimbali kukidhi mahitaji ya wateja

  • Ramani maalum, kulingana na ubunifu na vigezo vya mteja
  • Picha-ramani (orthophoto)
  • Muunganisho wa picha nyingi kuwa moja.
  • Ramani katika mfumo wa kompyuta
  • Ramani ya awali iliyochorwa kwa mashine za photogrammetry  Kumbukumbu Kuu ya Uoto kwa nchi nzima(katika mfumo wa kompyuta)
  • Picha za anga katika mfumo wa kompyuta kwa baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam

3.0 Huduma Mbalimbali

3.1   Upimaji

Idara    ina    uwezo    kivifaa    na kitaaluma kufanya upimaji wa aina mbalimbali

  • Upimaji miliki ukubwa wowote mahali popote nchini
  • Upimaji wa kuweka mifumo ya alama za msingi za upimaji
  • Upimaji kwa ajili ya utayarishaji wa ramani kutokana na picha za anga
  • Upimaji kwa kazi za uhandisi kama vile:
  • Miinuko na ubapa wa barabara 
  • Mapito ya njia za mawasiliano

3.2 Uchoraji na Uchapaji wa

Ramani

  • Tafsiri na utambuzi wa alama katika picha kwa madhumuni ya kuchora ramani, matumizi ya ardhi ama uoto juu-yake.
  • Uchoraji kwa mitambo ya photogrammetry
  • Usanifu wa ramani
  • Utoaji nakala za ramani au plani katika filamu kwa kamera maalum
  • Ukuzaji wa nyaraka kwa njia ya kamera hadi x6
  • Description: http://www.ardhi.go.tz/sites/default/files/clip_image002_0.jpg
    Kushona vitabu





















Uchapaji ramani

  • Kuchapa ramani katika rangi nyingi au moja hadi ukubwa wa 30" X 40"

3.3 Uwezo wa Kupima na Kuchora Ramani kwa Teknolojia ya Kompyuta.

  • Uchoraji wa ramani kwa kutumia mashine za photogmmmetry zilizoshikizwa na kompyuta
  • Uingizaji wa ramani katika kompyuta kwa njia ya board or screen digitization hadi ukubwa wa AO 
  • Upimaji ardhi kwa kutumia kifaa cha Total Station ambacho hunasa vipimo na takwimu moja kwa moja katika mfumo wa kompyuta 
  • Upimaji kwa taaluma ya anga za juu GPS
  • Kupata ramani ya umbile la ardhi kuonyesha mwinuko na mabonde usawa wa bahari
  • Upimaji wa mwinuko wa barabara
  • Usanifu wa ramani kwa kompyuta

Description: http://www.ardhi.go.tz/sites/default/files/clip_image002_2.jpg


UCHORAJI RAMANI KUTOKANA NA PICHA ZA ANGA

  • Kuchapa ramani kutoka kwenye kompyuta katika rangi moja au nyingi

4.    Teknolojia ya Kisasa

Kwa kutumia teknolojia ya kisasa, idara ina uwezo wa kuchora na kutoa ramani katika mfumo wa kompyuta. Ramani za baadhi ya maeneo hususan ya kati ya Jiji na Manispaa zote nchini ziko katika mfumo wa kompyuta. Ramani au Kumbukumbu Kuu ya Uoto wa Tanzania ipo katika mfumo wa kompyuta

5.    Upatikanaji wa Bidhaa na Huduma za Idara.


5.1   Huduma za Upimaji na

Ramani

Bidhaa za kawaida zikiwemo ramani, picha za anga huuzwa katika duka la ramani lililopo jengo la Casino katika makutano ya barabara za Kivukoni Front na Luthuli, jijini Dar es Salaam

5.2 Bidhaa na huduma ya pekee hupatikana kwa maombi ya mteja.

Kwa maelezo zaidi, wasiliana na:

Mkurugenzi,

Idara


No comments:

Post a Comment