Sunday, May 12, 2013

HIVI UNAFAHAMU TOFAUTI YA COLLEGE, UNIVERSITY NA INSTITUTE. HEBU SOMA UONE KAMA KUNA TOFAUTI KATI YAO.


Hebu tujaribu kuondoa utata wa maana ya majina haya yanayofanana kihuduma lakini kimuundo na yanayopatikana ndani yeke huwa ni tofauti.
CHUO(COLLEGE):
Kinatoa elimu na kuzawadia wahitimu shahada mbalimbali kwa kuegemea eneo moja tu la elimu. Mfano chuo cha biashara hutoa mafunzo yanayohusu biashara katika ujumla wake na haitagusa taaluma nyingine ya elimu zaidi ya biashara.

CHUO KIKUU(UNIVERSITY):
Kina mkusanyiko wa vyuo tofauti tofauti huku kila chuo kikiegemea eneo fulani la taaluma kwa jamii.
Mfano chuo kikuu cha Dar es salaam kina vyuo tofauti tofauti ndani yake vingine vikifundisha Ualimu, Biashara na hata Sayansi ya jamii.

TAASISI(INSTITUTE):
Ni chombo kinachotoa elimu ya ujuzi na inaweza pia kuwa sehemu ya chuo kikuu au taasisi nyingine za elimu ya juu na mara nyingi huwa ni mkusanyiko wa idara tofauti tofauti.

No comments:

Post a Comment