Sunday, May 12, 2013

JE, ULIWAHI KUHUDHURIA USAILI WA KAZI(JOB INTERVIEW)? YAFAHAMU MASWALI MAARUFU YANAYOPENDWA KUULIZA


UNADHANI KITU GANI NI KIGUMU ZAIDI KUWA MTENDAJI MKUU?


Hapa jikite zaidi katika mipango, utekelezaji, na gharama za usimamizi.
Elezea kuwa kazi kubwa kwa mtendaji mkuu ni kuwafanya wafanyakazi wake kufanya kazi kulingana na mipango ya ofisi, kuitekeleza kazi hiyo katika muda uliopangwa na pia ikamilike ikiwa imetumia bajeti iliyopangwa.

17.UNAUONAJE MWENENDO WA SOKO LA SHUGHULI ZETU?


Jiandae na vitu viwili au vitatu kuhusiana na mwenendo wa soko, na uonyeshe jinsi gani unalifahamu soko vizuri.
Unaweza ukagusia suala la changamoto za teknolojia au fursa, hali ya uchumi na hata mahitaji ya mamlaka zinazosimamia soko ili kuonyesha ni wapi soko la shughuli zenu linapoelekea.

18.SABABU GANI ZIMEKUFANYA UIACHE KAZI YAKO NA KUJA KUTAFUTA MPYA?


Elezea kwa kifupi sababu zako, kuwa mwaminifu pia bila kujiumiza wewe mwenyewe.
Waeleze kuwa kuondoka huko ulikuwa ni uamuzi wako, na wewe ni mtu wa kupenda kutafuta changamoto mpya na umeona sehemu sahihi ya wewe kuzipata ni hapa kwao.
Usije ukaelezea matatizo yako binafsi hapa, kwani unaweza ukajiharibia. Wanacholenga wasaili katika hili swali ni kujua kama ulifukzwa au uliondoka mwenyewe.

19.UMEJISIKIAJE KUACHA FAIDA ZA MAKATO YAKO KWA KUACHA KAZI ULIKOTOKA?


Waambie kuwa kiuhalisia uliguswa, lakini hukuwa na hofu.
Waambie kwamba ulikuwa tayari kuacha faida zote ili ukapate mazingira sahihi ya kazi ili uonyeshe kuwa maslahi si kipaumbele cha wewe kuajiliwa na wao.

20.KITU GANI ULIKUWA UNAKIPENDA, NA ULICHOKUWA UKIPENDI KATIKA KAZI YAKO ILIYOPITA?


Kuwa mwangalifu wakati wa kujibu hili swali, uwe na mtazamo chanya zaidi kwa kuelezea vitu vingi ulivyokuwa unavipenda kuliko ulivyokuwa unachukia.
Ukijifanya unataka kukosoa sana kazi uliyokuwa unafanya kabla ya kuja kuomba kwao, itawashangaza na kukuuliza kwanini uliendelea kubaki mpaka leo ndio uje kwao?

21.ULIKUWA UNAMUONAJE MKUU WAKO WA KAZI?


Hapa pia kuwa na mtazamo chanya, kwani hata kama mkuu wako hakuwa mwema kwako,
 ila jinsi utakavyomzungumzia kwa kuponda ndivyo muajili wako mpya atahisi utamfanyia yeye siku zijazo.

22.KWANINI UNAHISI HAUJAVUNA SANA KATIKA UMRI WAKO HUU?


Hapa waambie sababu moja kuu, ya kuwa ndio maana umekuja kwao kutafuta kazi 
na kuwa unajua thamani yako itapanda kupitia wao.
Usianze kujitetea sana hapa mpaka ukawaonyesha kuwa huna mipango mizuri na maisha yako.

23.UNADHANI KWA NAFASI UNAYOOMBA ULIPWE KIASI GANI?


Huu ni mtego mkubwa sana kwa wewe unayeomba kazi, unatakiwa uwe unafahamu viwango vya mishahara ya majukumu kama yako.
Endapo huyajui majukumu ya kazi yako, unaweza ukawauliza hapo hapo ili ukishayafahamu ndio uwatajie kiwango unachotaka.
Usije kujirahisisha au kujipandisha sana hapa, kwani nao wanaangalia kama uko kimaslahi zaidi  kuliko majukumu utakayopewa.
Au kuwatega na wewe, kama uliacha ajira mahali unaweza ukawaambia kuwa ulikotoka ulikuwa unalipwa kiasi fulani na ungependa kuona kiwango kinapanda.

24.UNA MIPANGO GANI YAKO YA MUDA MREFU?


Hapa wala usijisumbue na maelezo mengi, gusia kwa kifupi malengo yako ukiyahusianisha na malengo ya kampuni unayoomba.

25.UMEFANIKIWA KWA KIASI GANI MPAKA SASA?


Waeleze kuwa unajivunia na jinsi ujuzi wako unavyokua siku hadi siku.
Waambie pamoja na changamoto za kupanda na kushuka katika maisha lakini huna malalamiko na hatua uliyopo.
Hapa jionyeshe ni jinsi gani unajiamini na unafurahia unachofanya katika maisha yako.

HAYA NDIO MASWALI KUMI YALIYOKUWA YAMEBAKI AMBAYO NDIO HUWA YANAPENDWA KUULIZWA SANA WAKATI WA USAILI.

YAWEZEKANA KUNA MENGINE MENGI MAPYA UTAKUTANA NAYO LAKINI UNACHOPASWA KUFANYA NI KUJIANDAA KWA KUTUMIA PICHA ULIYOPATA KUTOKA KATIKA HAYA MACHACHE YA MIFANO.

HIVI UNAYATAMBUA MAMBO AMBAYO YAPO KICHWANI MWAKO NA YANACHANGIA KUKURUDISHA NYUMA? SOMA HAPA YATAMBUE NA UTAFUTIE UFUMBUZI WAKE LEO.


Moja kati ya vitu vigumu maishani, ni kuishi kama unavyotaka wewe maisha yawe.
Mara kwa mara utajikuta unachanganywa na vitegemezi kama chakula, manunuzi, matukio ya televisheni, mitandao ya kijamii na hata simu za mkononi.
Vitegemezi hivi vinachangia kukuondoa katika uhalisia wako wa maisha na kukusahaulisha hisia za kweli na unajikuta unapoteza fursa zilizopo.
Unapokuwa mpweke ndio unapata muda wa kuzitafakari hisia zako halisi kwa kina:
uoga, hofu, furaha, hasira, au hata huzuni.
Haijalishi hisia zako ni hasi au chanya lakini zinakupa picha halisi ya unataka nini katika maisha.

Tuangalie kwa pamoja sababu zinazochangia 
mpaka unapoteza fursa zilizopo:

1.KUTAKA KUFANYA KILA KITU:


Karibu kila binadamu kuna kipindi anahisi anapitwa na vitu vinavyofanyika duniani, ambavyo anatamani pia angekuwa anavifanya.
Lakini hakika unaweza ukazunguka kila sehemu na kutaka kujihusisha na kila kitu, mathalani  kufanya kazi,au burudani masaa 24  bila kulala lakini bado hautaweza kujihusisha na kila kitu.
Kwahiyo achana na hisia za kwamba unapitwa na mambo na tambua kila unachotakiwa kufanya kipo katika mazingira yako.

2.KUKWEPA MAUMIVU NA KUSHINDWA:


Usijaribu kuukimbia ukweli wa maisha yanayokukabili, kwani maumivu na kushindwa ndio vitu vinavyosaidia ukuaji wako wa akili.
Kumbuka, kuna tofauti kati ya kuwa katika mazingira ya kushindwa na kuwa umeshindwa tayari .
Hautaweza kuvikimbia vitu hivi mpaka viwe vimekufundisha unachopaswa kukijua katika maisha yako, ili uchukue hatua nyingine mbele.

3.KUENDELEA KUSHIKILIA KUMBUKUMBU ZA ZAMANI:


Usijaribu kutumia muda wako mwingi kufikiria mambo mabaya ambayo yalishapita kwani kufanya hivyo ni kuyaruhusu yaharibu wakati uliopo.
Usijaribu kuishi wakati mwengine, unatakiwa ukubali kumaliza hizo kumbukumbu ili uanze kujenga mwanzo mpya.
Anza kufunga kumbukumbu za mambo mabaya ya zamani sasa na jua hayatakuongoza unapotaka kufika.

4.KUJIKUMBUSHIA MATUKIO YA KUSHINDWA:


Kama ukiendelea kujisimulia historia za matukio uliyoshindwa kichwani mwako, utayaamini na kujiona ni mtu wa kushindwa daima.
Swali ni: Historia unayojisimulia inakutia nguvu?
Usiendelee kuweka makosa yako kichwani, kwani uzito wake utaangusha uwezo wako halisi.
Unapaswa utambue kuwa kila kitu mwanzo huwa ni kigumu kabla hakijawa rahisi.

5.KUIGIZA MAISHA YA MWENGINE:


Vita kali zaidi uliyowahi kupigana nayo ni vita ya kutaka kuwa wewe, hivyo ulivyo sasa.
Hautawezi kuwa wewe kama kila siku unajitafuta kwa watu wengine.
Kumbuka, unapoigiza maisha ya mtu mwengine unapoteza nafasi ya kujitumia wewe mwenyewe na uwezo wako wa asili utakufa kwa kuwa hautumiki.

6.PICHA YAKO KICHWANI YA UNAVYOTAKA VITU VIWE:


Moja kati ya vitu vinavyokuangusha katika maisha ni picha unayoijenga kichwani 
na kutaka kila kitu kiwe kama ulivyokiona wewe mawazoni.
Maisha yanasonga na mara kwa mara sio kama ulivyotaka yawe, bali kadri yalivyopaswa yawe.
Maisha ni kama muziki unaochezwa ambao haukuuchagua, lakini unaweza ukachagua namna ya kuucheza.

7.KUJIONA UNA KASORO:


Usijihukumu mwenyewe, kuna watu wengi wanatamani kufanya hiyo kazi kwa ajili yako.
Fanya unayopaswa kufanya kwa uwezo wako na mengine yanayobaki yasalimishe kwa wengine.
Jipende na jionee fahari na kila kitu unachofanya hata kama umekosea kwani hata makosa yanaonyesha ulijaribu kufanya.

8.KUENDELEA KUSUBIRI:


Acha kuendelea kuisubiri kesho, kwani muda wa leo hautaupata tena.
Maisha ni mafupi sana kama kila siku unaomba udhuru.
Achana na mitazamo ya kutaka kufanya kila kitu kesho, anza leo kufanya hatua japo moja ya jambo lako kwa ujasiri.
Kama huna hakika ni njia gani hasa unayopaswa kupita, kufuata moyo wako ndio njia bora iliyobaki.

KAA TAFAKARI NI JAMBO LIPI KATI HAYO HAPO JUU LIMEKUWA TATIZO KWA WEWE KUFIKIA MALENGO YAKO.

ANZA KULISHUGHULIKIA SASA NA UTAONA MATUNDA YAKE.


Ukimaliza Chuo nani atakuajiri?


Arusha. Mawazo ya wahitimu wengi wa vyuo nchini katika miaka ya karibuni  imekuwa ni namna ya kupata  ajira zenye tija.
Ndoto ya wengi ni kupata kazi za kipato kizuri na ambazo zitawawezesha kuishi vizuri, kumiliki gari, kujenga nyumba na mambo mengine lukuki.
Hata hivyo, baadhi wamekumbana na tatizo la ajira ambalo limewasukuma katika kubuni miradi ambayo  itawawezesha kumudu maisha na changamoto zake.
Mmoja wao, Simon Kinabo, mhitimu wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kilichoko Morogoro ameamua kujiajiri baada ya  kubuni mradi wa  ufugaji wa samaki.

Mradi huo  unaoitwa Rombo Unique Aquaculture, upo kilomita 60 kutoka mjini Moshi na kilomita nne kutoka makao makuu ya Wilaya ya Rombo, eneo la Mkuu.
Anasema akiwa mwanafunzi katika chuo hicho, akisomea Shahada ya Sayansi ya Viumbe wa Majini (BSc Aquaculture) alihamasika na somo la uzalishaji wa samaki na ndipo akaamua kuanzisha mradi huo kwa mtaji wake.

“Katika fedha zile za mkopo,  kila nikipewa na Serikali, nilichukua kiasi kidogo na kuanzisha nyumbani mradi wa kufuga samaki.
Niliamini ni mradi mzuri ambao unaweza kubadili maisha yangu,” anasema.
Anaongeza kuwa alianzisha mradi huo  kwa kuchimba bwawa dogo na kuanza kuzalisha samaki, kwa lengo la kuja kuwauza baadaye.

Mkopo wa CRDB
Anasema akiwa mwaka wa pili SUA  alipata taarifa ya kuwapo mradi wa SUGECO unaoendeshwa na chuo hicho na CRDB ambao unalenga kuwawezesha wanafunzi wa elimu ya juu kuingia katika ujasiriamali.

“Baada ya kupata taarifa hizo nilijitokeza kuandika andiko la kuomba fedha na baada ya usaili, andiko langu lilipitishwa na chuo na CRDB,” anasema.
Anaongeza kuwa baada ya kupitishwa andiko lake, alipokea mkopo wa Sh20 milioni kwa ajili ya kuanzisha mradi.

Baada ya kupokea fedha, aliamua kupanua bwawa  hilo na pia kuliongezea mifumo ya kuingiza maji kutoka Mto Ngwasi na kutoamaji ili liwe la kisasa.
“Nilinunua mabomba 100 ya futi 2,000 na sasa bwawa langu lina urefu chini, mita  tatu hadi sita na upana mita 30,” anaeleza.

Anasema kuwa baada ya upanuzi wa bwawa alinunua samaki wadogo 3,000 kutoka Gereza la Karanga mjini Moshi ambao walikuwa ni  wa jamii ya perege na kambare.
Anaongeza kuwa  kila kifaranga cha samaki alikinunua kwa Sh300 na kwamba hiyo ilikuwa Mei 5, mwaka  jana, alipoanza kuwapandikiza bwawani mwake.

Mafanikio ya mradi
Hadi sasa, Kinabo anasema bwawa lake linao  zaidi ya samaki  40,000, kati ya hao wakubwa ni 10,000 na wadogo 30,000.
Anasema , Juni mwaka huu  anatarajia kuanza kuvua samaki na  matarajio yake  ni kuvua tani  nne  za samaki.
“Nina imani tani hizo nne, nikivua naweza kupata zaidi ya Sh60 milioni na tayari nimepata masoko,” anasema  msomi huyo.

Anasema tayari, amefanya mazungumzo na wakuu wa shule kadhaa za sekondari  wilayani Rombo, Hospitali ya wilaya hiyo na maeneo kadhaa ambao wamekubali kununua samaki wake.
Kwa kutambua kuwa hawezi kufanya kazi  hizo peke yake, mjasiriamali huyo msomi amemwajiri mtunza mazingira, James Edmund,  pia hivi karibuni atakuwa na walinzi wawili na muuzaji wa samaki.

Dodoma. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetangaza kuwa wakati wowote itakamilisha mchakato wa kufuta hati za mashamba ya mikonge yaliyotelekezwa katika Wilaya za Muheza na Kilindi mkoani Tanga.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Goodluck Ole-Medeye wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilindi Dastan Kitandula (CCM).
Ole Medeye alisema kuwa uamuzi wa kufuta hati miliki hizo kwa sasa uko mikononi mwa Rais baada ya kukamilika kwa hatua zote.
Katika swali hilo Kitandula alitaka kujua ni lini Serikai itafuta hati miliki kwa mashamba ya mkonge ambayo kwa muda mrefu yametelekezwa ili kuwagawia wananchi wenye uhitaji.
Awali, Herbert Mtangi (Muheza-CCM) alitaka kujua ni viwango gani stahiki ambavyo wawekezaji wa zao la katani wanatakiwa kulipa kama ushuru kwa halmashauri husika.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Hawa Ghasia, alisema kuwa halmashauri zote nchini zimepewa mamlaka ya kutoza ushuru wa mazao chini ya kifungu 7 (1) (g) cha sheria ya fedha za serikali za Mitaa.
“Ushuru huu hulipwa na mununuzi na unatozwa mahali ambapo zao linazalishwa na kwa bei ya mkulima yaani bei ya zao kabla ya kuongezwa thamani,” alisema Ghasia.
Alisema wafanyabiashara wote wa zao la mkonge,wanatakiwa kulipa ushuru wa mazao ambao ni kuanzia asilimia 3 hadi 5 kwa mujibu wa sheria.
Wakati huohuo, Naibu Waziri wa Maji, Dk Binilith Mahenge amemtetea bosi wake, Profesa Jumanne Maghembe kuhusu tuhuma zilizoelekezwa kwake za kupeleka mradi mkubwa wa maji jimboni kwake, huku wilaya zingine zikiachwa ‘yatima’.
Akijibu hoja mbalimbali za wabunge jana, Dk Mahenge alisema mradi wa Mwanga-
Same-Korogwe ni mwendelezo wa miradi mikubwa ya maji kama ule wa Chalinze.
“Yote yaliyoelezwa tutayazingatia. Ni kweli kutokana na unyeti wa suala la maji, lazima hisia zitapelekea mawazo mengi juu ya kasungura kadogo kuonekana mtu mmoja amejimegea wengine hakuna,” alisema Dk Mahenge.


Soda ni SUMU

JUMATANO, MEI 08, 2013 05:13 NA FRED OKOTH
*Utafiti wabaini ina kiwango kikubwa cha kemikali hatari mwilini mwa binadamu

Utafiti wa wanasayansi mbalimbali duniani unaonesha kuwa kuna madhara makubwa ya utumiaji wa vinywaji aina ya soda katika mwili wa mwanadamu
AFYA za mamilioni ya Watanzania wanaotumia vinywaji vya aina ya soda ipo hatarini, baada ya kugunduliwa uwepo wa chembechembe zenye kemikali za sumu ndani ya vinywaji hivyo, MTANZANIA Jumatano linaripoti.

Utafiti uliofanywa na Muungano wa Waandishi wa Habari za Uchunguzi Tanzania (Investigative Journalists Union of Tanzania- IJUTA) pamoja na tafiti zilizofanywa na wataalamu waliobobea katika afya ya umma duniani, umebaini kuwa vinywaji baridi aina ya soda ni hatari kuliko utumiaji wa sigara inayosababisha maradhi ya kansa katika mwili wa binadamu.
Kwa mujibu wa utafiti wa wanasayansi mbalimbali duniani, yapo madhara makubwa ya utumiaji wa vinywaji vya aina ya soda katika mwili wa binadamu.
Utafiti huo unaonyesha kuwa zipo sababu nane kuu zinazokiweka kinywaji aina ya soda kwenye kundi la vinywaji vyenye sumu ambavyo havifai kwa matumizi ya binadamu.

IJUTA imebaini kuwa makampuni makubwa yanayotengeneza vinywaji baridi aina ya soda yanatumia mabilioni ya dola kila mwaka kujitangaza na kutoa misaada ya kijamii kutokana na mauzo yake, bila kutaja madhara ya vinywaji hivyo kwa binadamu.

Kwamba matangazo hayo yanayogharimu mamilioni ya fedha ndiyo yanayokifanya kinywaji hicho kuwa maarufu zaidi duniani, licha ya kuwa na madhara makubwa katika mwili wa binadamu.

Aidha, utafiti huo unaonyesha kuwa umaarufu mwingine wa kinywaji aina ya soda ni utamu wa kupindukia ulio ndani ya soda.

Utafiti wa IJUTA unaonyesha kuwa utamu wa kupindukia iliomo ndani ya soda unawapumbaza wanywaji ili wasisikie ladha kali ya asidi iliyomo ndani ya soda.

IJUTA imegundua kuwa kiwango cha asidi kilicho ndani ya soda hakiwekwi wazi kwa walaji kwa sababu ya kuhofia kuwa wakibaini wataacha kikutumia kinywaji hicho.

Inaelezwa pia kuwa madini ya cola yaliyo ndani ya soda yana kilevi aina kafein kinachomteka mnywaji kuwa teja wa kinywaji hicho.

Tafiti za kitaalamu zimeonyesha kuwa soda inahusishwa na matatizo mengi ya kiafya kwa watoto na watu wazima, yakiwemo matatizo ya kuongezeka unene kupita kiasi, ugonjwa wa ini na mengineyo.

Utafiti uliofanywa nchini Marekani unaonyesha kuwa soda huwekewa ‘fructose’ (sukari) nyingi kupitia mfumo wa sirapu (fructose corn syrup) ambayo inaongoza kwa kusababisha magonjwa ya unene, kisukari, ugonjwa wa moyo na magonjwa mengine sugu yanayowakabili Wamarekani wengi hivi sasa na dunia kwa ujumla.

Dk. Mercola, ambaye ni mtaalamu wa masuala ya lishe asilia na tiba mbadala nchini Marekani, amekaririwa na tafiti mbalimbali zilizofanyika nchini humo akieleza kuwa kinywaji aina ya soda ni hatari kwa binadamu, sawa na mtu anayevuta sigara au zaidi, jambo alilosisitiza kuwa siyo la kutia chumvi, bali ukweli halisi.

Watumiaji wa vinywaji aina ya soda wanaelezwa kuwa wamekuwa wakinywa kiasi kikubwa cha kaboni, kafeini (dawa ya kulevya), sukari ya kupundukia na asidi kali ambayo huvuruga afya ya mtumiaji kwa kiwango cha juu.

Soda pia imebainika kutokuwa na lishe ya aina yoyote zaidi ya maji na sukari.

Uchunguzi wa IJUTA na utafiti ya wanasayansi mbalimbali duniani, umeonyesha kuwa watu wengi hawajui kuwa unywaji wa soda huwaongezea kiasi kikubwa cha madini joto.

Chupa moja ya soda yenye ujazo wa mililita 330 husababisha unene kwa kiwango cha paundi moja kwa mwezi.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kisukari Tanzania (TDA), Ramadhan Mongi, amepata kukaririwa na vyombo vya habari hapa nchini akieleza kuwa ugonjwa wa kisukari Tanzania umeongezeka mara sita katika siku za hivi karibuni.

Alisema miaka kumi iliyopita, hali ya kisukari ilikuwa asilimia tatu (3), lakini katika miaka ya karibuni umeongezeka mara sita.

“Tunastahili kuongeza jitihada ya kupambana na gonjwa hili la kisukari kwa gharama zote kwa sababu kisukari ni moja ya magonjwa manne yanayomaliza Watanzania,” alisema.

Utafiti uliofanyika Mkoa wa Dar es Salaam ulibaini kwamba kati ya watu watano waathirika wa kisukari, mmoja tu ndiyo hupata matibabu ya serikali.

Unywaji kwa mpigo wa kabohaidrets iliyo na sukari nyingi kwenye soda hudhoofisha seli zinazozalisha vimeng’enya tofauti na vyakula vingine na pia imebainika kuwa sukari ikiingia kwa wepesi kwenye mzunguko wa damu husababisha kongosho kuzalisha vimeng’enya vingi mwilini.

Uchunguzi wa kitabibu katika Hospitali ya wanawake ya Boston nchini Marekani na katika Chuo cha Kitabibu cha Harvard umeonyesha wanawake 51,000 hawakuwa na kisukari mwanzoni mwaka wa 1991, lakini miezi minane baadaye wanawake 741 waligundulika na kisukari.

Ripoti ya utafiti huo ilionyesha kuwa wanawake waliokuwa wakitumia kinywaji aina ya soda moja ama mbili
kwa siku waliongezeka uzito maradufu na walikuwa hatarini kupata ugonjwa wa kisukari.

Pia ilionyesha kuwa soda hudhoofisha mifupa na husababisha hali ya mifupa kupuputika, hali inayomuweka mtumiaji kuwa katika hatari ya kuvunjika mifupa kirahisi.

Madhara mengine yaliyobainika kusababishwa na unywaji soda ni kupukutika kwa meno na ama kuoza. Pia soda husababisha matatizo ya figo.

Soda yenye chembe ya cola husababisha figo kuwa na mawe kwa sababu ya asidi na kemikali mbalimbali zinazofichwa vipimo vyake kwa walaji.

Madaktari bingwa wa wanamichezo wanaeleza madhara yanayosababishwa na soda mwilini kuwa ni pamoja na shinikizo la damu, uharibifu wa ini, huvurugu mfumo wa kumeng’enya chakula tumboni kutokana asidi ya kiwango cha juu iliyo kwenye soda.

Wanashauri kuwa soda haistahili kutumika kama kishawishi kwenye mchezo, kwa sababu ina madhara makubwa kwa wanamichezo kwa sababu hunyonya maji kwenye mwili na kudhoofisha mwili.

Wakati utafiti huo ukidhihirisha hayo, Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeshindwa kutoa tamko lolote kuhusu utafiti huo, hata baada ya kupelekewa maswali kwa maandishi yanayoomba ufafanuzi wa ubora wa vinywaji vya soda katika mwili wa binadamu.




Jumatano, Mei 15, 2013 05:22 Na Fred Okoth
*Yakatazwa shuleni, watoto chini ya miaka 12
*Sasa yabainika kuwa ina sumu inayoua taratibu
*Yagundulika kupumbaza na kusababisha uteja

SIKU chache baada ya gazeti hili kuripoti madhara yanayosababishwa na kinywaji aina ya soda, katika utafiti wake gazeti hili limebaini mengine mapya.
Kwa mujibu wa utafiti huo, imebainika kuwa soda imepigwa marufuku kutumiwa na watoto walio na umri chini ya miaka 12 na walio shuleni katika baadhi ya mataifa ya Ulaya na Marekani, kutokana na madhara ya kiafya yanayosababishwa na kinywaji hicho.


 



Taarifa zilizotolewa na Shirika la Habari la The Press Television Technology Advertising and Branding (Adweek) zinazonukuu taarifa ya kampuni moja kubwa duniani inayozalisha kinywaji aina ya soda, imeamua kupambana na unene (obesity), unaosababishwa na unywaji wa soda kwa kuondoa matangazo ya vinywaji vyake kwenye vyombo vya habari.

Kampuni hiyo kupitia taarifa yake hiyo iliyotolewa katika moja ya sherehe zake, ilieleza kuwa lengo la kuondoa matangazo hayo ni kuwanusuru watoto wadogo na matumizi ya vinywaji aina ya soda vilivyobainika kuwa na madhara katika mwili wa binadamu.

Nchini Marekani, tayari imekwishapitishwa sheria inayokataza watoto walio na umri wa chini ya miaka 12, kunywa kinywaji aina ya soda.

Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, alieleza kuwa mipango ya mbeleni ya kampuni yake ni kutengeneza kinywaji hicho kikiwa na kiwango kidogo cha Kalori na kubuni kinywaji cha aina hiyo ambacho kitakuwa hakina Kalori.

Alisema mipango hiyo itatekelezwa duniani kote ambako kinywaji cha aina ya soda kinatengenezwa na nchini Marekani tayari imekwishaanza kutekelezwa.



Aidha, Kampuni hiyo imeahidi kuweka wazi virutubisho vyote vinavyotumika kutengeneza bidhaa zake na kuahidi kutoa misaada ya hali na mali kwa nchi zote 200 duniani ambako kinywaji cha soda kinauzwa.

Mbali na Marekani, kinywaji cha aina ya Soda kimekwishapigwa marufuku shuleni katika nchi za Uingereza, Ufaransa na katika majimbo ya Los Angeles, Philadelphia na Miami nchini Marekani na kwa watu wazima matumizi yake yanaelekezwa kuwa ya kiwango kidogo sana.

Vyombo vya habari vya nchini New Zealand, mwezi Machi mwaka huu viliripoti kuwa mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Natasha Harris (31), alifariki kutokana na unywaji wa soda nyingi.

Shirika la habari la AFP la Ufaransa, liliripoti tukio hilo kwa kueleza kuwa Natasha alikuwa akinywa soda nyingi kila siku, jambo ambalo liligeuka kuwa sehemu ya maisha yake kwa kipindi cha miaka mingi.

Kwamba familia ilikuwa ikimuita teja wa soda, baada ya meno yake kuoza kwa sababu ya kunywa soda, alijifungua mtoto ambaye hakuwa na fizi jambo ambalo liligundulika baadaye kuwa lilisababishwa na matumizi makubwa ya kinywaji hicho.

“Tumegundua kwamba, kwa kuzingatia ushahidi uliopo, kama sio unywaji wa soda uliopitiliza, Natasha Harris asingekufa katika muda ule na katika hali alivyokufa

“Ripoti ya Daktari aliyechunguza maiti yake (Pathologia), iligundua kwamba ini lake lilipanuka sana, likawa na mrundiko mkubwa wa mafuta kutokana na kula sukari kwa wingi. Kuwepo kwa madini aina ya ‘potasiam’ kwa kiwango kidogo sana kwenye damu yake, pia kulitokana na unywaji wa soda.” Taarifa ya kitabibu katika Hospitali aliyofia nchini New Zealand ilieleza.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kisayansi zilizo kwenye mitandao ya wanasayansi waliobobea duniani, unywaji wa soda humpumbaza mtumiaji na kumsahaulisha kula vyakula vyenye madini muhimu mwilini.

Moja ya andishi linalotahadharisha utumiaji wa kinywaji cha soda na kukitaja kuwa cha hatari kwa matumuzi ya binadamu, ni Jack Winkler, Profesa wa sera za lishe katika Chuo Kikuu cha Metropolitan nchini London, linaloeleza kuwa Soda ni bidhaa ya kishetani inayoua binadamu taratibu baada ya kinywaji hicho kumzalishia magonjwa mengi mwilini yanayomfanya kuwa tegemezi wa dawa.

Wakati msomi huyo akieleza hayo katika utafiti wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Dk. Raymond Wigenge, amelieleza gazeti hili soda siyo kinywaji hatari kwa matumizi ya binadamu kwa sababu kinatumiwa na mamilioni ya watu duniani kote.

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano ofisini kwake wiki iliyopita baada ya kutoa ufafanuzi kuhusu madhara yanayosababishwa na kinywaji aina ya soda katika mwili wa binadamu, Dk. Wigenge alisema pamoja na changamoto zilizopo katika kinywaji hicho, taasisi yake haipingi uwepo wa kinywaji hicho sokoni.

“Soda haina shida kwa binadamu na hata mkiendelea kuandika suala hili, sisi tutaendelea kuueleza umma kwamba waendelee kupata kinywaji, hivyo kama ambavyo tumekuwa tukifanya,” alisema.

Alipoulizwa kama anakubaliana na tafiti za wanasayansi bingwa wa magonjwa ya binadamu walioeleza katika tafiti zao kuwa unywaji wa soda una madhara katika mwili wa binadamu, alisema hizo ni changamoto za kawaida, kwa sababu madhara yaliyomo kwenye soda hayamuathiri mtu mara moja bali huchukua muda mrefu.

Wakati Dk. Wigenge akieleza msimamo wake kuhusu kinywaji aina ya soda, nchini Mexico, taasisi ya El Poder del Consumidor inayojihusisha na kutetea walaji, inashinikiza Serikali ya nchi hiyo kuzilazimisha kampuni za soda kuorodhesha madini na chembechembe zote za kemikali zinazotumika kutengeneza kinywaji hicho.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Alejandro Calvillo, amekaririwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo akieleza kuwa unywaji wa soda ni hatari na hilo limethibitishwa na wataalamu wa afya duniani kuwa soda ni sumu mbaya, inauwa taratibu.

Tafiti mbalimbali za wanasayansi zinaeleza kuwa soda ina asidi aina ya ‘phosphoric’ yenye uwezo wa kuvuruga madini ya ‘calcium’ yaliyoko mwilini na kusababisha mifupa na meno kudhoofika.

Aidha, asidi aina ya ‘phosphoric’ huvuruga asidi aina ya ‘hydrochloric’ iliyo tumboni mwa binadamu na hivyo kuharibu mfumo wa kusaga chakula.

Viwanda vya soda ndio watumiaji wakubwa wa sukari na wanasayansi wanasema sukari hupandisha kiwango cha ‘insulin’ ambayo husababisha kasi ya mzunguko wa damu, ugonjwa wa moyo, kupanda kwa ‘Cholesterol, kisukari, kuzeeka mapema, ongezeko la uzito na maradhi mengine.

Aidha inadaiwa kuwa viwanda vya soda pia hutumia dawa ya kulevya aina ya kafeini. Wataalamu wanasema vinywaji vyenye kafeini, husababisha kupanda kwa mapigo ya moyo, kasi ya mzunguko wa damu na matatizo ya kizazi.





HIVI UNAFAHAMU TOFAUTI YA COLLEGE, UNIVERSITY NA INSTITUTE. HEBU SOMA UONE KAMA KUNA TOFAUTI KATI YAO.


Hebu tujaribu kuondoa utata wa maana ya majina haya yanayofanana kihuduma lakini kimuundo na yanayopatikana ndani yeke huwa ni tofauti.
CHUO(COLLEGE):
Kinatoa elimu na kuzawadia wahitimu shahada mbalimbali kwa kuegemea eneo moja tu la elimu. Mfano chuo cha biashara hutoa mafunzo yanayohusu biashara katika ujumla wake na haitagusa taaluma nyingine ya elimu zaidi ya biashara.

CHUO KIKUU(UNIVERSITY):
Kina mkusanyiko wa vyuo tofauti tofauti huku kila chuo kikiegemea eneo fulani la taaluma kwa jamii.
Mfano chuo kikuu cha Dar es salaam kina vyuo tofauti tofauti ndani yake vingine vikifundisha Ualimu, Biashara na hata Sayansi ya jamii.

TAASISI(INSTITUTE):
Ni chombo kinachotoa elimu ya ujuzi na inaweza pia kuwa sehemu ya chuo kikuu au taasisi nyingine za elimu ya juu na mara nyingi huwa ni mkusanyiko wa idara tofauti tofauti.